Gavana Tunai aponea kifo katika ajali ya helikopta

Gavana wa Narok Samuel Tunai na wengine watatu walinusurika katika ajali ya helikopta Jumamosi alasiri.

Gavana Tunai alikuwa ametoka mazishi ya marehemu Paul Lepore katika kijiji cha Olenkipejus huko Melili, Kaunti ya Narok wakati wa tukio hilo.

Marehemu alikuwa baba wa Julius ole Sasai ambaye anafanya kazi kama Waziri wa Fedha katika Baraza la Mawaziri la Gavana Tunai.

Gavana na watu wengine watatu waliokuwamo kwenye helikopta hiyo walitoroka bila kujeruhiwa lakini wakakimbizwa katika kituo cha afya cha karibu kukaguliwa.

Bado haijulikani ni nini kilichosababisha helikopta hiyo kuanguka.

Scroll to Top